MJADALA WA HITIMISHO LA MAFUNZO YA ISAVET CHUO KIKUU CHA SUA, MOROGORO
Siku hiyo ilikuwa ya jua kali huku upepo mwanana ukivuma kutoka milima ya Uluguru, ukichangia hewa safi na baridi pembezoni mwa ukumbi wa mikutano uliopo Chuo Kikuu cha Kilimo na Mifugo (SUA) mkoani Morogoro. Hapa ndipo mjadala muhimu uliohusu hitimisho la mafunzo ya In-Service Applied Veterinary Epidemiology Training-ISAVET yaliyoandaliwa na FAO Tanzania ulifanyika.
Washiriki walikusanyika kwenye moja ya kumbi ndogo za mikutano pembezoni mwa ukumbi mkuu wa mikutano, kujadili mafanikio na changamoto za programu hiyo.
Ufunguzi wa Mjadala:
Dr. Moses Ole Neselle kutoka FAO, akiwa ni msimamizi wa programu hiyo, alianza kwa shukrani za dhati kwa washiriki wote waliohudhuria na kwa mchango wao muhimu katika mafunzo hayo.
“Mafunzo ya ISAVET yamelenga kuboresha ufuatiliaji na usimamizi wa magonjwa ya mifugo. Leo tuko hapa kujadili tuliyojifunza na jinsi tunavyoweza kuboresha zaidi katika siku zijazo,” alisema Dr. Neselle kwa msisitizo.
Ushuhuda wa Washiriki:
Bi. Asha Zahran, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mifugo kutoka Zanzibar, alikuwa wa kwanza kutoa maoni yake. Alielezea jinsi mafunzo yalivyoboresha ufuatiliaji wa magonjwa huko Zanzibar. “Kupitia mafunzo haya, tumeweza kuboresha mfumo wetu wa taarifa za magonjwa na kuweka mikakati madhubuti ya kudhibiti magonjwa yanayotishia mifugo yetu,” alisema Bi. Asha kwa shauku.
Fusebia Mussa, mshiriki wa mafunzo kutoka Wilaya ya Tanganyika, alisimama na kutoa ushuhuda wake. “Kupitia haya mafunzo hakika nimeongeza ujuzi mkubwa na nitakapo rejea kituoni kwangu nitafanya mabadiliko makubwa hususani katika ufuatiliaji wa magonjwa ya mifugo, na ikiwa nipamoja na uchukuaji wa hatua za kuyadhibiti,” alielezea Fusebia akionyesha matumaini makubwa baada ya program hiyo.
Bi. Wantere Maswe kutoka Kituo cha Mifugo cha Ramadi wilayani Busega, alieleza jinsi mafunzo hayo yanavyoweza kumsaidia katika kuboresha ushirikiano kati ya wakulima na wataalamu wa mifugo. “Mafunzo haya yamenifundisha mbinu za kuwasiliana vizuri na wakulima, na sasa tutafanya kazi pamoja kwa karibu zaidi kuhakikisha mifugo yetu inabaki na afya njema,” alisema Bi. Wantere kwa tabasamu.
Mjadala ulipofikia mwisho, Dr. Neselle alitoa hitimisho lake, akiwapongeza washiriki kwa mchango wao mkubwa. “Tumepata mengi kutoka kwa kila mmoja wenu. Haya mafunzo yameonyesha umuhimu wa ushirikiano na ufuatiliaji thabiti.
Tunahitaji kuendelea kuboresha mifumo yetu na kushirikiana kwa karibu zaidi, hata hivyo ni muhimu tuendelee kujifunza na kubadilishana taarifa. Pia, tunahitaji kuhakikisha mafunzo haya yanakuwa endelevu na yanafikia maeneo mengi zaidi, hususan vijijini,” alisema Dr. Neselle.
-
7:49:44
Akademiks
1 day agoKendrick Lamar - Not Like Us Video Breakdown - Rick Ross Reacts to Beatdown. Foolio Ressurected?
184K41 -
52:43
Talk Nerdy 2 Us
11 hours agoDigital Defense: Unraveling Major Cyber Attacks and Protecting Your Data
60.9K4 -
1:21:33
The Quartering
18 hours agoBiden's Desperate Interview, Disney ROASTED By Gina Carano, Ballot Boxes RETURN The Fix Is In!
136K83 -
1:45:53
Robert Gouveia
20 hours agoTrump Offers to SAVE Biden! Donors THREATEN Campaign; BRUTAL Report DESTROYS Joe
136K168 -
1:21:11
Russell Brand
21 hours ago‘THE US IS FALLING APART’ - EXCLUSIVE Colonel Douglas MacGregor Interview (and UK Elections) - 401
331K425 -
51:33
Ben Shapiro
19 hours agoEp. 1998 - Is TONIGHT The Night Biden Drops Out?
165K125 -
19:25
Neil
19 hours agoAs Everyone's Distracted With The NEW UK GOVERNMENT... (A LOT's About To Change...)
106K25 -
1:02:14
Geeks + Gamers
21 hours agoGina Carano DESTROYS Mark Ruffalo And Disney Double Standard, Japan Is FURIOUS Over Assassin's Creed
110K35 -
1:13:29
Steve-O's Wild Ride! Podcast
3 days ago $0.18 earnedPenguinZ0 Has No Respect For Dr. Disrespect! - Wild Ride #222
106K11 -
2:00:57
LFA TV
1 day agoMERRY INDEPENDENCE! | LIVE FROM AMERICA 7.5.24 11am EST
126K59